Msingi wa ukuaji bora unazingatia kwanza kujitambua mwenyewe na kisha aina ya maarifa unayopokea...
Ili uweze kufanikiwa unahitaji sana kukua katika maeneo matano tofauti ( Imani,Hisia,Akili,Kijamii na Uchumi) ukuaji huu unahitaji mwongozo sahihi ili uweze kufikia kilele cha mafanikio na malengo yako.
Uhalisia wa maisha kwa sasa unahitaji umakini zaidi kwenye kufanya maamuzi zaidi ya ilivyokuwa awali, wazee wetu walitumika sana kuchukua nafasi ya washauri ( Consultants & Mentors ) , hii ilipelekea kutengeneza mzani sawia kati ya asili, heshima, maadili, kazi nakadhalika kwa sababu jamii iliangalia sana kupata maelekezo na uwezo kutoka kwa wazee wetu, lakini kwa sasa mambo yamebadilika muingiliano wa IMANI, TAMADUNI, UTANDAWAZI na TEKNOLOJIA.....Aina za ukuaji tunazojihusisha nazo moja kwa moja.
Kukua Kiuchumi
Kukua Kiakili
Kukua Kiimani
Kukua Kijamii
Kukua Kihisia
kwa hatua sahihi
Kupitia Fursa Foundation utaweza kupata huduma ya ushauri kwa masuala mbalimbali ikiwemo imani, maisha, biashara, uchumi na mahusiano. Haya ni maeneo ambayo vijana wengi wameshindwa kuvuka salama aidha kwa kukosa uangalizi sahihi ama maarifa sahihi ya kufikia malengo yao.
Soma Zaidi
Kupitia Fursa Foundation tunatoa pia semina mbalimbali kwa vijana,wazazi,familia, shule na makanisa kwa ujumla, semina kwa ajili ya kujitambua na maarifa kwa watu wote kwani changamoto ya maarifa sio ya pande moja ukimuelimisha baba na mtoto hana elimu tambua kutakuwa na mvutano hivyo kupitia Fursa Foundation utaweza kuwa na semina ya familia ambayo itaruhusu wanafamilia wote kujumuika na kupata elimu pamoja, lakini hata kwa ngazi nyingine lengo ni kukua kwa hatua sahihi.
Soma Zaidi
Kupitia Fursa Foundation tunatoa semina kozi za mafunzo ya ufundi stadi ili kuongeza ujuzi na maarifa kwa watu, ufundi stadi ni mbadala mzuri wa kipato chako ukiwa na maarifa ya kufanya vitu vingi maana yake ni unakuwa na fursa nyingi zaidi, tunatoa mafunzo kulingana na ratiba na mpangilio wa kalenda ya mwaka hivyo endelea kuwa karibu na mitandao yetu ama acha namba za simu sehemu ya mawasiliano nasi tutakujulisha kwa wakati sahihi.
Soma Zaidi
Fursa Foundation tunatoa msaada wa hali na muda mwingine mali, kulingana na uhitaji lakini pia uwezo wa huduma, matarajio yetu ni kutatua changamoto zilizoko ndani ya uwezo wetu kwa wale wanaotufikia kwa msaada zaidi ya ushauri na ushauri wa kitaalam zaidi.
Soma zaidiBaadhi ya maswali na majibu kwa ufahamu zaidi wa Fursa Foundation na jinsi unavyoweza kunufaika na ushirika nasi.
Una swali zaidi