Fursa Foundation - Kua kwa hatua sahihi.
Uhalisia wa maisha kwa sasa unahitaji umakini zaidi kwenye kufanya maamuzi zaidi ya ilivyokuwa awali, hapo awali wazee wetu walitumika sana kuchukua nafasi ya washauri ( Consultants & Mentors ) kwa vijana wa rika mbali mbali , hii ilipelekea kutengeneza mzani sawia kati ya asili, heshima, maadili, kazi nakadhalika kwa sababu jamii iliangalia sana kupata maelekezo na uwezo kutoka kwa wazee wetu.
Lakini kwa sasa mambo yamebadilika muingiliano wa IMANI, TAMADUNI, UTANDAWAZI na TEKNOLOJIA vimepunguza sana nafasi ya wazee kuwa muhimili wa jamii, kwa sasa jamii imegeukia imani, tamaduni,utandawazi na teknolojia kuwa msingi kwa kiasi kikubwa kupitia mafundisho ya imani,mtindo wa maisha ya tamaduni fulani, utu na maadili ya utandawazi pia mwongozo wa teknolojia. Vitu hivi vimeleta changamoto kwenye namna sahihi ya kuyaendesha maisha yetu huku kukiwa na asili ambazo tumezirithi kwenye damu ambazo hazihitaji muingiliano, hii imepelekea madhara kadha ambayo yamebadili na kuathiri kila nyanja ya makuzi bora.
Fursa General Enterprises Ni kampuni ya kizalendo iliyosajiliwa BRELA - 621358, chini ya chapa yake FURSA FOUNDATION tunakaona ipo haja ya kusaidia jamii kuweza kutatua baadhi ya changamoto ambazo zinamlengo chanya hasa kwa watoto na vijana ambao ndio wako kwenye hatari kubwa ya uathiri wa makuzi, malezi na mazingira ( Mtindo wa maisha), ndipo tukakuanzishia chapa maalum kwa ajili ya kutatua changamoto hasi na kuzifanya ziwe chanya.
Baadhi ya maswali na majibu kwa ufahamu zaidi wa Fursa Foundation na jinsi unavyoweza kunufaika na ushirika nasi.
Una swali zaidi